Mwaka 2023 staa wa Amapiano Bongo, Chino Kid alifanya kazi na mkali wa Hip Hop Fidq, kupitia ngoma ya ‘kibabe’, 2024 Chino anaanza fresh kwa kuzama studio na Mwanamba wa Kaskazini Joh Makinitz na hii ilikuwa ni ndoto yake, amesema chino.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Chino ame-share picha na videos zinazowaonyesha wakiwa studio na kuandika “KUSEMA UKWELI HII MOJA YA NDOTO KUBWA SANA KWENYE MAISHA YANGU YA KISANAA NA NAJUWA ITAKUWA NDOTO YA VINAJA WENGINE WENGI KUFANIKISHA KUFANYA KAZI NA WEWE MKUBWA MWAMBA @johmakinitz
SO IMEKUWA KAMA BLESS KWANGU NA KATIKA KUELEKEA SIKU MUHIMU SANA KWANGU PALE KIDIMBWI TAREHE
4/2/2024”
