
NA EUNICE KANUMBA-SHINYANGA
Aliyekuwa mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga, Azza Hillal Hamad leo tarehe 30 june 2025 amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kugombea jimbo jipya la Itwangi ambalo lilikatwa kutoka katika jimbo la Solwa mkoani Shinyanga.
Azza amekabidhiwa fomu hizo katika ofisi ya CCM wilaya ya Shinyanga vijijini na katibu wa wa wilaya Elenestina Richard.