Hayawi hayawi sasa yamekuwa hatimaye mwanadada Ashanti na Nelly wanatarajia mtoto wao wa kwanza pamoja.

Mtandao wa PEOPLE, umethibitisha hilo. Utakumbuka baada ya kuachana mwaka 2013 mapema mwezi Septemba wawili hao waliweka wazi kurudia baada ya kujificha ficha kwa muda mrefu toka 2013.
Mtoto huyu atakuwa ni mtoto wa kwanza kwa Ashanti na wa Tatu kwa rapa Nelly, ambaye anamtoto wa kike na wakiume (Chanelle Haynes(29), Cornell Haynes III(24)), watoto hao alizaa na mwanamama aitwaye Channetta Valentine.


