Kampuni ya boti ya Venezia Turismo Motoscafi, kupitia msemaji wake imelaani kitendo cha rapa Kanye West na mkewe Bianca Censori walichofanya kwenye boti yao na kusema ni Uchafu mtupu na wamempiga marufuku kutumia usafiri huo.
Msemaji anasisitiza kuwa dereva wa boti hakuona uchafu huo kwa sababu alikuwa akiendesha boti hiyo na kama angeona basi angeripoti mara moja kwa mamlaka husika.
Tukio hilo la kupasuka kitako linatajwa kuwa ni kiki ya kuitangaza albamu mpya ya Kanye West.