Baada ya Harmonize_tz kudai kuwa kuna wasanii wanawatia ujinga wasanii ambao wamepita lebo yake ya Konde Gang, Anjella_tz ameijubu kauli ya aliyekuwa Boss wake huyo kupitia Instastory yake.
“Broh safari gani uliyobariki? Wakati unapiga simu kuzioa riziki zetu pale tunapojitafuta… wewe ndio wakwanza usiopenda mafanikio yetu au niweke Ushahidi?,” amendika Anjella.
Anjella ni miongoni mwa wasanii waliowahi kusainiwa lebo ya Konde Gang mwaka 2021, mwaka 2023 msanii huyo alijiengua lebo hiyo kwa sababu mbalimbali.