Staa wa muziki Naira Marley , ametua nchini Nigeria kwaajili ya kusaidia polisi uchunguzi wa kifo cha rapa Mohbad kilichotokea Septemba 12/2023.
“Ningependa kuwataarifu kuwa nimerejea hivi punde Lagos, Nigeria ili kusaidia mamlaka na uchunguzi unaoendelea. Ni muhimu nifanye sehemu yangu kwa Imole. Nitakutana na polisi, na ni matumaini yangu kuwa ukweli utafichuka na haki itatendeka,” amendika staa huyo kwenye mtandao wa Twitter (X)