Categories

Do you have a Story?

Call us on 0677 644 444 to submit your news story or incident report!

Wakili akwamisha kesi ya watuhimiwa 8 wa ugaidi Shinyanga

Mahakama kuu ya Tanzania inayoshughulikia makosa ya rushwa na uhujumu uchumi iliyoketi katika masijala ya Shinyanga leo Septemba 7 2023 imeahirisha kusikiliza mashahidi upande wa Jamuhuri katika kesi no 3 ya uhujumu uchumi na ugaidi ya mwaka 2023 inayowakabili watuhumiwa 8 waliokamatwa mwaka 2017 wilayani kahama kufuatia mmoja wa mawakili wa upande wa utetezi kutofika mahakamani .

Katika kesi hiyo washitakiwa wote 8 wanakabiliwa na makosa 6 ya ugaidi ikiwa ni pamoja na kupanga njama ya kufanya vitendo vya kigaidi, kuajiri watu kwa ajili ya kufanya ugaidi huku mshitakiwa namba 2 na namba 8 wakikabiliwa na tuhuma za kufadhili fedha ambazo zingetumika katika vitendo vya kigaidi na mshitakiwa namba 1 na namba 8 wakikutwa na hatia ya kushiriki vikao vinavyohusishwa na vitendo vya kigaidi wakati wakijua ni tishio kwa umma.

Watuhumiwa hao wote ni wakazi wa Kahama na kesi itaendelea tena Septemba 8 2023 kwa kuwasikiliza mawakili upande wa Jamuhuri.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *