Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa ambaye pia ni Waziri Mkuu wa Tanzania na Dkt. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU).
Viongozi hao, wamezungumza jambo wakati wakiagana baada ya kikao cha mashauriano kilichofanyika hii leo Aprili 11, 2025 ofisini kwa Balozi Nchimbi, Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma.
Katika Picha kushoto ni John Mongella, Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara).

