MWANAFUNZI AJINYONGA BAADA YA KUFELI KIDATO CHA NNE..

Msichana aitwae Rabia Poul (19) Mwanafunzi wa Kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Nyanza Mkazi wa Mtaa wa Barabara ya Msalala Manispaa ya Geita Mkoani Geita amefariki Dunia kwa kujinyonga February 11 Mwaka huu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, SACP Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akisema chanzo cha kifo cha Mwanafunzi huyo ni kufeli Mtihani wa Kidato cha Nne.

Jongo amesema ‘Binti amejinyonga hadi kufa na tukio hili limetokea siku ya tarehe 11 februari 2025, chanzo cha tukio hili ni baada ya Mwanafunzi huyo kugundua kwamba amefeli kidato cha nne kwa kupata Division 0’ – RPC Jongo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *